Tafuta katika Blogu Hii

Ijumaa, 15 Februari 2019

WANAWAKE WAJASIRIAMALI MKOANI KILIMANJARO WAHIMIZWA KUTUMIA FURSA




Wito umetolewa kwa Wanawake wajasiriamali mkoani Kilimanjaro kutumia fursa zilizopo ikiwemo kutekeleza kwa vitendo taratibu,kanuni na sheria  zilizokwa na Serikali ili kujikwamua kiuchumi
Hayo yamebainishwa na mkuu wa mkoa wa Kilimanjaro Mh.Anna Mghwira kufuatia ufunguzi wa kikao cha wanawake wajasiria mali na wafanyabiashara mkoani hapa kilicholenga kuimarisha mahusiano,kubadilishana ujuzi na kuunda mtandao wa kibiashara katika ustawi wa uchumi, familia na taifa kwa ujumla.
Mghwira amesema katika ustawi wa viwanda wanawake wanashiriki asilimia kubwa kuhakikisha huduma muhimu za kijamii zinapatikana na kuongeza chachu ya ushindani unaozaa matunda katika kukuza uchumi  ikiwemo kuimarisha mahusiano  miongoni mwa mtu binanfsi ,vikundi,makampuni na taasisi  mbalimbali .
Akifafanua zaidi amesema dhamira na kipau mbele cha  Mhe.  Rais John Pombe Magufuli kuifanya  Tanzania kuwa nchi ya viwanda ,wajasiriamali wanapaswa kuviwezesha viwanda vidogovidogo  vikue katika ustawi mzuri kwa kuzingatia upatikanaji wa  mali ghafi na soko la uhakika .
  Serikali inawategemea sana ninyi wajasiriamali katika kutekeleza kauli mbiu hii ya mheshimiwa rais katika  kubadilika kifikra, kuwa na uthubutu na hatimaye kukuza uchumi wa nchi yetu ,Sisi kama mkoa na Serikali kwa ujumla tutaendelea kushirikiana na sekta binafsi kuhakikisha kunakuepo na mazingira bora na rafiki  kwa wajasiriamali katika mkoa  wetu. ” alisema Mkuu huyo wa mkoa.
Katika hatua hiyo Mhe. Mghwira amezitaka taasisi za kifedha kuboresha mikopo nafuu kwa wajasiriamali wadogowadogo kwa kuzingatia uhalisia wa biashara zao na marejesho sambamba  na mamlaka husika kuwa waadilifu na kuepuka mianya ya rushwa .
Wakati huohuo Mwenyekiti wa Chama cha wanawake wafanyabiashara(TWCC)mkoani hapa Bi.Joyce Ndosi amesema wanafanya jitihada mbalimbali kuzikamilisha ndoto za wanawake wajasiriamali kuimarika  kiuchumi na kijamii licha ya kukabiliwa na changamoto mbalimbali ikiwemo usafirishaji wa bidhaa nje ya mipaka ya nchi na upatikaji wa masoko .
 “Mwanamke ni nguzo ya familia hivyo kujituma na kujishughulisha na biashara ni msingi wa ustawi wetu katika kuhakikisha familia zetu pamoja na jamiii inakuwa salama, hivyo TWCC ni jukumu letu kupaza sauti na kuongeza hamasa kwa wanawake kutokua tegemezi na kupata wigo mpana katika uwajibikaji sambamba na kuzifanya changamoto kuwa fursa kuzichangamkia fursa katika kukuza uchumi wa nchi.” alisema Ndosi.




Hakuna maoni:

Chapisha Maoni