Tafuta katika Blogu Hii

Jumamosi, 16 Machi 2019

SERIKALI YAAHIDI KUTUMIA BUSARA KUUMALIZA MGOGORO BAINA YA SBL NA RAHCO.

Picha inayohusiana
Pichani ni Naibu Waziri wa Viwanda na Biashara Eng.Stella Manyanya

Naibu Waziri wa Viwanda na Biashara, Stella Manyanya amesema  serikali kupitia wizara yake itatumia busara kumaliza mgogoro uliopo kati ya Mamlaka ya Reli hapa nchini (Rahco) na kiwanda cha Serengeti Breweries (SBL) kuhusu kubomolewa nusu ya eneo la kiwanda hicho.
Akizungumza wakati wa ziara yake fupi ya siku moja  mkoani Kilimanjaro iliyolenga kutembelea viwanda vilivyobinafsishwa na  Serikali  ambapo aliambatana  na kamati ya kudumu ya Bunge  ya Viwanda ,Biashara na Mazingira  iliyolenga kubaini uhalisia wa mgogoro baina ya Shirika hilo na kiwanda hicho.
Manyanya amesema Serikali inatambua mchango mkubwa unaofanywa na  wawekezaji haowa SBL kupitia sekta ya viwanda ikiwemo kuongeza pato la taifa sambamba na kuitangaza Tanzania katika Nyanja mbalimbali ikiwemo Utalii wa ndani na nje .
“Jina la kiwanda hiki ni sehemu moja wapo ya kuitangaza Tanzania kwa upande wa utalii  kupia mbuga yetu  ya wanyama Serengeti, SBL wamekua ni wadau wazuri baada ya kubinafsishwa, ni walipa kodi wazuri na waaminifu kwa Serikali yetu na niwapili kwa sasa kiukubwa kwa utoaji wa huduma ya vinywaji aina ya pombe hivyo tunafurahi kuona  baadhi ya viwanda tulivyovibinafsisha kikiwemo kiwanda hiki vinaendelea vizuri zaidi hususani katika swala zima la usafi  katika ngazi ya kimataifa”
Amesema uwekezaji uliofanywa katika kiwanda hicho una tija kubwa kwa wananchi katika ustawi wa uchumi kama ilivyo azma ya Serikali yetu hivyo kupitia ziara hii tumekutana na changamoto ya mgogoro wa ardhi baina ya Mamlaka ya  reli hapa nchini  na kiwanda hicho ambapo kimsingi reli hiyo bado haijajengwa.
“Ardhi ipo ya kutosha ,hivyo tutakaa nawizara zote zinazohusika na jambo hii na kupata suluhu,najua hili halina tatizo, nipende kuwatoa shaka wawekezaji wetu busara itatumika na mambo yatakwenda vizuri.Huyu mwekezaji yuko ‘Serious’tunapenda kuona anaendelea kuwepo hivyo nchi hii ipo kwa ajili ya kuangalia maslahi mapana na mchango unaofanywa na  wawekezaji hawa,”amesema Manyanya.
Kwa upande wake Mwenyekiti wa kamati ya Bunge ,Viwanda ,Biashara na Mazingira,Suleiman Sadiki ambaye pia ni Mbunge wa Mvomero amesema mgogoro huo unahitaji suluhu ya haraka zaidi kwasababu unashirikisha wawekezaji wawili akiwemo wa ndani na nje ya nchi.
“Wawekezaji hawa tunawakatisha tama kwa namna moja au nyingine na nia ya kamati hii ya Bunge  ni kuunga mkono juhudi mbalimbali za Rais katika kuelekea Tanzania ya Viwanda ,Tumekutana na changamoto hii ya mgogororo wa ardhi ambapo tumekutana na mambo makuu matatu moja Uwepo wa kesi iliyopo Mahakamani,pili Barua ya kubomoa ukuta na tatu ni Kutokuwepo kwa barua inayoonyesha kuwa mgogoro huo umeisha hivyo kama kamati tumeyabeba haya yote tunakwenda nayo,  kazi yetu kubwa ni kuishauri Serikali katika ustawi wa viwanda ili tuangalie namna ya kulimaliza jambo hili kwa haraka kwasababu miongoni mwa viwanda vinavyochangia pato la taifa kwa kulipa kodi ni Kiwanda hiki cha Serengeti Brewieris “alisema Sadick.
Akifafanua zaidi amesema kupitia nyaraka mbalimbali za hati za kiwanja hicho zilizopo wataishauri vyema serikali kuumaliza mgogoro huo mapema iwezekanavyo bila ya kuathiri uhusiano wa kibiashara  kwani enoo la reli mpaka kufikia kuta za kiwanda hicho  lina ukubwa wa kilometa moja”Wawekezaji hawa wametuambia wana hati mbili ikiwemo ya eneo lenye mgogoro huo lakini tulipowauliza wenzetu wa Rahco wamesema hawana hati ya eneo hilo”alisema Sadick.
Kwa upande wake Mkurugenzi wa Mawasiliano SBL John Wanyancha amesema wanaishukuru Serikali ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania  kupitia  Kamati hiyo ya Bunge kwa kuipa kipau mbele sekta ya viwanda hivyo wanaiomba Serikali kuhakikisha eneo hilo halibomolewi kutokana na uhitaji mkubwa wenye tija kwa wananchi ikiwemo ajira kwa wazawa ,fursa kwa wakulima mbalimbali wakiwemo wa zao la  Mahindi,Shairi na Mtama.
                          FUATILIA TUKIO HILI HAPA BILA KUKOSA.
 
Pichani aliyetangulia mbele kabisa ni Mkurugenzi wa Mawasiliano wa SBL John Wanyancha akiwa ameambatana na viongozi mbalimbali kiwandani hapo.

Aliyetangulia mbele ni Mkuu wa Wilaya ya Moshi Kippi Warioba akiwa ameambatana na Timu ya Kamati ya Bunge na Viongozi mbalimbali wa Serikali.
Hapa ni ndani ya kiwanda cha Serengeti Bweries (Moshi) Wajumbe wanatembelea kuona hali halisi.
Hii ni moja ya alama iliyopo mbele kabisa ya kiwanda hicho.
Aliyenyoosha mkono ni Mkurugenzi wa Mawasiliano Bw.John Wanyancha akiwaonyenya wajumbe wa kamati ya Bunge na Viongozi juu ya eneo linalodaiwa kuwa litabomolewa kupisha ujenzi wa reli .

Hapa ni nje ya kiwanda cha SBL-Moshi na hii ni barabara kuu ya Moshi -TPC hatua chache tu kutoka kwenye geti  la kiwanda hicho.
Wajumbe wa Kamati ya Bunge Viwanda,Biashara na Mazingira wakijadiliana kidogo baada ya kuona uhalisia eneo husika n a thani ya Miundombinu.