Tafuta katika Blogu Hii

Jumamosi, 23 Machi 2019

RC DKT.MGHWIRA AWAONYA WATENDAJI WA UMMA ,AKERWA NA UONEVU KWA WAFANYABIASHARA.




KULIA NI MWENYEKITI WA CCM MKOA WA KILIMANJARO BW.PATRICK BOISAFI ALIYESHIKA KIPAZA SAUTI NI MKUU WAMKOA WA KILIMANJARO DKT.ANNA MGHWIRA ANAYEFUATA NI KATIBU TAWALA MKOA ENG.AISHA AMOUR.

Mkuu wa Mkoa wa Kilimanjaro Dkt.Anna Mghwira amezitaka Mamlaka husika zinazoshughulikia uhuwishwaji wa taarifa muhimu za kiutendaji kutimiza wajibu wao kikamilifu ili kuepuka migogoro isiyo na tija  baina yao na walaji sambamba na kuchukua hatua  stahiki katika kutoa huduma za kiada na ziada.
Rai hiyo imetolewa kufuatia mkutano maalumu wa Wafanya biashara mkoani humo uliolenga kuchakata na kutatua  kero mbalimbali na fursa zinazopatikana ndani ya mkoa katika kukuza uchumi na ustawi wa biashara .
Mghwira amesema ni vyema taasisi za Umma zilizopewa dhamana kujitathimini kwa kina ili  kuyafikia malengo yaliyokusudiwa katika  kuboresha mfumo wa utoaji huduma muhimu zilizokusudiwa na kuondoa dhana hafifu zinazo ambatanishwa na itikadi za kisiasa kupitia kada mbalimbali  kwa baadhi ya wananchi juu ya utendaji wa Serikali yao. “Wafanyabiashara wanailalamikia Mamlaka ya Mapato TRA kwa kuwanyanyasa na wakati mwingine kuahidi kuzisimamisha huduma mbalimbali pasipo kuzingatia misingi ya haki , mazingira,wajibu kinga ya kisheria na kuwakandamiza wafanyabiashara kulipa faini mbalimbali tofauti na dhamana walizopewa kuelimisha wadau juu ya huduma mbalimbali na jinsi ya kutatua changamoto zinazowakabili Serikali inafuata misingi sahihi ya uwajibishaji wa waalifu pasipo kujali itikadi za vyama wala dini ”alisema Mghwira.
Akipokea  moja ya hoja kutoka kwa wafanyabiashara wanaotekeleza wajibu wao katika Stendi kuu ya Mabasi Moshi wawekezaji hao  wameilalamikia Halimashauri ya Manispaa ya Moshi kupandisha kodi ya vibanda kutoka sh.30,000 kwa mwezi hadi kufikia Sh.400,000 mara baada ya mkataba wa uwekezaji kuisha mnamo 31/12/2018.
Wakifafanua zaidi wawekezaji hao wamesema tozo hiyo ni kubwa hivyo inawaumiza waliowengi na kuonekana kutotambulika kwa jitihada walizozionyesha kuiunga mkono Serikali   katika ujenzi wa vibanda hivyo ambapo awali waliwekeza katika jengo hilo na kuchangia  ujenzi wa Sh.4.5Milioni .
Akijibu hoja hiyo Mghwira amesema hatokubali Serikali ipakwe tope kutokana na uamuzi huo wa Manispaa  kwani kwa kufanya hivyo ni kuonyesha dhahiri kuwa Serikali imeshindwa kutambua na kuthamini  mchango na uwepo wa wafanyabiashara hao .
“Hii kodi mliyoiweka  ni kubwa mno ,mmeenda mbali kwa  kutoza kodi kwa kiwango hiki ,mnachokifanya mnajenga hoja ,mnataka kusema Serikali imeshindwa kutothamini  michango ya wafanya biashara hawa waliojitoa miaka 15 iliyopita kuchangia ujenzi wa jengo lile, ikumbukwe mtu aliyechangia ujenzi  ni tofauti na mtu anayekuja na dau kubwa ambaye hajachangia ujenzi wa miundo mbinu yoyote” amesema Mghwira.
Hata hivyo  Ameitaka  Manispaa ya Moshi kupitia Mstahiki Meya Raymond Mboya na Mkurugenzi Bw.Michael Mwandezi kutathimini na kuziangalia baadhi ya huduma zinazolalamikiwa na wawakezaji hao  katika eneo la Stendi Kuu ya Moshi ikiwemo  tozo kubwa  la pango  hali inayosababisha kudhorota kwa hali ya kibiashara na huduma hafifu kwa walaji.
“ Mbali na kuwepo kwa mgogoro unaoendelea katika jengo hilo kwa miaka mingi hivi sasa naiagiza Manispaa  ya Moshi kukaa meza moja na wafanyabiashara ili kutatua mgogoro huu mapema  iwezekanavyo  sambamba na kupanga viwango vipya vya kodi,fuateni vigezo na viwango vilivyopo sokoni,soko hili ni huria sio holela ,wekeni bei ambayo haitawaumiza wafanyabiashara  hawa wanamchango mkubwa sana katika jengo lile  ”amesema Mghwira.
                                         
                                  TIZAMA PICHA ZA MNATO KATIKA TUKIO HILO.
          
PICHANI NI MKURUGENZI WA KAMPUNI YA  CHRISBURGER BW.CHRIS SHAYO AKICHANGIA HOJA KATIKA MKUTANO HUO.

PICHANI NI MSTAHIKI MEYA MANISPAA YA MOSHI BW.RAYMOND MBOYA AKIJIBU HOJA.

PICHANI NI KAMANDA WA UHAMIAJI MKOA WA KILIMANJARO BW.ALBERT RWELAMILA AKIJIBU HOJA.
WA KWANZA KABISA PICHANI ALIYEVAA MIWANI NI AFISA UHUSIANO WA KIWANDA CHA SUKARI TPC-MOSHI  BW.JAFARY MICHAEL.
PICHANI NI MAAFISA WA CRDB BENKI BW.LUDOVICK NGOWI NA ADAM MGAZA WAKIFATILIA HOJA KWA MAKINI.
PICHANI NI WADAU WAKIFUATILIA HOJA MBALIMBALI KATIKA MKUTANO HUO.
PICHANI NI MWENYEKITI WA DALADALA MANISPAA YA MOSHI BW.SAIDI SELEMANI AKICHANGIA HOJA KUHUSIANA NA SUMATRA.
MUWAKILISHI KUTOKA TAASISI YA OSHA  BI.WINNIE KIWELU AKITOA HOJA KATIKA MKUTANO HUO.
PICHANI NI BAADHI YA WADAU WAKISIKILIZA HOJA KWA MAKINI KATIKA MKUTANO HUO.
WA KWANZA PICHANI MKURUGENZI WA KAMPUNI YA HARSHO GROUP BW.HAROLD SHOO  ANAYEFUATIA NI  MKURUGENZI WA DEMA CONSTRUCTION BW.DISMAS MASALU ALIMAARUFU (DEDE)
PICHANI NI AFISA WA SIDO BI .LILIAN MATERU AKIJIBU HOJA ZA WAJASIRIAMALI.
WAWAKILISHI KUTOKA NMB BENKI WAKIFUATILIA HOJA KWA MAKINI.

PICHANI NI MKURUGENZI WA KAMPUNI YA DORKIA ENTERPRRISES BI. DORCAS KIBONA AKITOA HOJA KUHUSIANA NA SIDO.

PICHANI NI MKURUGENZI WA MANISPAA YA MOSHI BW.MICHAEL MWANDEZI AKIJIBU HOJA.

PICHANI NI MJUMBE THOMAS MAKYAO AKICHANGIA JAMBO.