Tafuta katika Blogu Hii

Jumanne, 23 Aprili 2019

KAMATI YA ULINZI NA USALAMA MKOANI KILIMANJARO YAAHIDI KUWASHUGHULIKIA ASKARI POLISI WANAODAIWA KUWANYANYASA NA KUWAFYETULIA RISASI WANANCHI WA KIJIJI CHA SANYA STATION KILICHOPO WILAYANI HAI


Mkuu wa Mkoa Wa Kilimanjaro Dkt.Anna Mgwhira Akizungumza Katika Mkutano Wa Hadhara Uliofanyika Katika Kijiji cha Sanya Station kilichopo Wilayani Hai na Kinachopakana na Uwanja wa Ndega Kia.

Serikali mkoani Kilimanjaro imeagiza uchunguzi  ufanyike dhidi ya askari polisi wanaodaiwa kuwanyanyasa na kuwatesa wananchi wanaoishi katika kijiji cha Sanya Station kinachopakana  na uwanja wa ndege  wa Kia Wilayani Hai.
Wakizungumza katika mkutano wa hadhara uliohudhuriwa na viongozi mbalimbali wa kamati ya ulinzi na usalama mkoani humo wanakijiji hao wameeleza kunyanyaswa  ikiwemo kutumbukizwa kwenye maji machafu ,kutukanwa na  kubaguliwa na askari hao sambamba na kuwafyetulia risasi sizizo na tija katika maeneo wanayoishi  na kuhatarisha maisha yao .
Wakifafanua zaidi wamesema wamekuwa wakikamatwa  na mifugo yao,kufedheheshwa na kuwekwa chini ya ulizi basipo sababu za msingi na kutakikana kutoa rushwa ya pesa  tasilimu ili kuachiwa huru au kufunguliwa kesi ambazo zinazowagharimu kutumia muda wao mwingi kuhudhuria Mahakamani na kushindwa kuendesha shughuli za uzalishaji.
Kwa upande wake mkuu wa mkoa wa Kilimanjaro Dkt.Anna Mgwhira ameeleza kusikikitishwa na baadhi ya watumishi wa jeshi la polisi kuwanyanyasa wananchi  na kuagiza askari hao watambuliwe na kuchukuliwa hatua  kali za kisheria .
Hata hivyo Kamanda wa Polisi mkoani humo Bw.Hamisi Issa amesema hayupo tayari kuona wananchi wanafedheheshwa na kufanyiwa vitendo vya kikatili na askari wanaodaiwa kutenda tukio hilo na kuahidi kuwatambua askari waliohusika haraka iwezekanavyo na hatua zaidi za kisheria kufuata mkondo wake.

Katika Picha Ni Wanakijiji wa Sanya Station Wakiwasikiliza Viongozi mbalimbali Waliofika Katika Mkutano huo.
Pichani Ni Mwenyekiti wa Kijiji Cha  Sanya Station  Akitoa ufafanuzi Juu Ya Wananchi Wake Wanavyopata Adha Kutoka .

Katika Picha Ni Mkuu Wa Wilaya Ya Hai Mhe.Lengai Ole SabayaAkitoa Maelezo Ya Kina Juu Ya Mgogoro Huo.