Tafuta katika Blogu Hii

Alhamisi, 9 Mei 2019

MBOWE AKERWA NA KAULI YA RC MAKONDA AMWAGA POVU KATIKA MISA YA MAZISHI YA DKT.MENGI.


Pichani ni Mwenyekiti wa Chama cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema), Freeman Mbowe

Mwenyekiti wa Chama cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema), Freeman Mbowe amewataka Watanzania kutogombanishwa na baadhi ya kauli za viongozi zisizonatija na kuleta mipasuko katika jamii  husani katika itikadi za  kikabila na kidini huku akiwataka viongozi kutafakari maneno wanayoyateta kwani yanaweza kugawa watu na kuleta machafuko katika jamii.


Aidha, Mbowe ambaye pia ni Mbunge wa Hai,  amemuelezea aliyekuwa Mwenyekiti wa Kampuni za IPP, Dk. Reginald Mengi alikuwa ni mtu asiyekata tamaa,asiyejivuna na mwenye busara kwa kila mtu hata wale masikini wa chini kabisa aliwapa heshima licha ya kuwa alikua tajiri.

Mbowe ameyasema hayo Punde tu wakati akitoa salamu za rambirambi katika ibada ya kumuaga aliyekuwa Mwenyekiti Mtendaji wa Kampuni tanzu za IPP, Dk. Reginald Mengi iliyofanyika katika Kanisa la Kiinjili la Kilutheri Tanzania (KKKT), Moshi Mjini mkoani Kilimanjaro.

“Kuna kauli zinasemwa sana na watu kwa ukweli zinakera kwa vile mimi Mbowe  si mnafiki lazima niseme na nitasema hapa hapa mbele za watu kwa lengo lakuimarisha utaifa na sio itikadi za chama,udini   au ukabila".

“Tuna nchi moja ambayo tunastahili kupendana na kusaidiana, na kila mtu ana haki ya kumsaidia mwenzie, tusikubali kauli za viongozi zitugawe  hasa za kidini na kikabila, kauli ya kusema kuna makabila hayawezi kuwasaidia walemavu si nzuri na haikutupendeza kwa kweli, tujitafakari tunapotaka kuongea maneno ,” amesema Mbowe.

Aidha Mbowe ametoa wito kwa kila aliyeguswa na msiba wa Dk. Mengi kuyaenzi yale yate aliyokuwa akiyatenda enzi za uhai wake kwani hiyo ndiyo alama  pekee aliyoyuachia na hatuna budi kumuenzi.

“Mzee Mengi ameshatangulia mbele za haki haitajalisha tuzungumze mema kiasi gani kumuhusu hatutamrejesha, ila tujitafakari na kuyaenzi yale aliyokuwa akiyafanya, alikuwa mnyeyekevu na kauli zake zilijenga, kupatanisha na kuleta matumaini lakini pia hakuwahi kukata tamaa,” amesema Mbowe.



Hakuna maoni:

Chapisha Maoni