Tafuta katika Blogu Hii

Alhamisi, 9 Mei 2019

MSIBA WA MENGI WAGEUKA DARASA KWA VIONGOZI WA UMMA :WAZIRI MKUU KUWAONGOZA MAELFU YA WATANZANIA .


Waziri Mkuu Mhe.Kassim Majaliwa akiweka shada la maua katika kaburi alilozikwa Dkt. Mengi.
Waziri mkuu wa Tanzania Kasimu Majaaliwa, ameongoza maelfu ya watanzania katika mazishi ya aliyekuwa mfanyabiashara maarufu  ukanda wa Afrika mashariki, Dr. Regnald Mengi, ambaye amezikwa leo katika makaburi ya familia nyumbani kwa wazazi wake kijiji cha Kisereni Machame mkoani Kilimanjaro Km 35 kutoka Moshi mjini.

Akitoa salamu za rambi rambi kwa niaba ya Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania , Waziri Mkuu Kassim Majaaliwa amesema kuwa taifa litamkumbuka Dkt. Mengi kwa mchango wake mkubwa wa kukuza uchumi nchini hasa katika sekta ya madini, habari, viwanda na mazingira, kwani amewahi kuwa mwenyekiti wa abaraza la mazingira Taifa.

 Waziri mkuu Majaaliwa amesema mchango wa Dkt.Mengi katika kuwakumbuka watu wenye mahitaji maalumu utaendelea kukumbukwa daima kuindokewa na mtu mzalendo katika historia ya Tanzania

"Hakuna Mtanzania asiyejua mchango alioutoa kwa Taifa hili,kwa namna alivyoguswa katika nyanja mbalimbali kwa jamii na hata kwa serikali, tunatambua mchango wake"alisema Majaliwa.

Amesema kuwa kama Taifa la Tanzania  msiba huo wa Dkt Reginald Mengi alikuwa ni mtu wa upendo na hakuwa na ubaguzi hivyo pigo na wameondokewa na mtu aliyekuwa muhimu maishani na Mungu alimbariki na yeye akawa baraka kwa wengine.

 Akitoa mahubiri katika ibada ya mazishi hayo iliyofanyika katika kanisa la Kiinjili la Kilutheli Tanzania KKKT Usharika wa Moshi mjini, Askofu mkuu wa Kanisa hilo Dkt. Fredrick Shoo, amewaasa viongozi wa serikali hasa wale wenye umri mdogo kuacha kiburi cha madaraka na badala yake watende haki kwa wananchi wote bila upendeleo na watapata za Mungu.

Dkt Shoo amemtaja Marehemu Mengi kuwa  hakuwabagua maskini japo alikuwa na tajiri na tabia hiyo inapaswa kuigwa na watu wote wenye nafasi za uongozi serikalini, wenye madaraka na wenye pesa.

Askofu Dkt. Shoo asisitiza kuwa kama Taifa la Tanzania linahitaji kupokea baraka kutoka kwa Mungu ni muhimu kuacha  ubaguzi,  kiburi na kujikweza,amekemea baadhi ya tabia ya kauli za viongozi ambazo zinaweza kuleta migogoro katika jamii.

Kwa upande wake mwenyekiti wa chama kikuu cha upinzania nchini Tanzania Freeman Mbowe, amekemea tabia ya ubaguzi wa ukabila unaooneshwa na baadhi ya viongozi na kwamba ili kumuenzi Mengi ni muhimu kuyaacha matendo hayo kwani alikuwa ni mtu wa kujishusha japo alikuwa Bilionea.

Katika hatua nyingine Askofu Dkt.Shoo amewataka Watanzania kuacha tabia ya kubaguana kwani ni dhambi mbele za Mungu ,wenye nafasi kuwakandamiza wale walio wa hali ya chini,amewataka kuacha kiburi 

"Hivi nyie viongozi haswa vijana mnapopata cheo mnajisahau wanaojitutumua kama chatu wakumbuke kuwa kila siku tunamuomba Mungu na lazima Mungu  atawashusaha"

Kwa upande wake Waziri mkuu Kassimu Majaliwa ametoa pole kwa familia ya Marehemu Dkt.Regnald Mengi kwa kuondokewa na mpendwa wao,amesema amepokea kwa mshtuko mkubwa taarifa ya msiba wa Mengi

Tujifunze kuwathamini  watu wasio na uwezo katika jamii na Taifa kwa ujumla msikivu ,mpenda amani,na mwenye kuwasaidia wengine 1990 alianza kupata chakula cha pamoja na watu wenye ulemavu.

Kwa upande wake Mkuu CCM Taifa  Bashiru Ally amesema mchango wa Dkt. Mengi katika Taifa haswa katika mazingira  alisisitiza kupanda na kuotesha mingi tumuenzi na kupanda miti ya kutosha

"Baba Askofu hatujafanya kazi ya kuwaandaa vijana wetu kuwa Viongozi bora, sasa tunavuna matunda yake, naomba nimuombe msamaha kijana wangu Makonda, nilimsema Simiyu mara ya kwanza, akaja ofisini analia, ameanza kujirekebisha" alisema Bashiru

Akitoa salamu kwa niaba ya Bunge Spika wa Bunge la Tanzania Job Ndugai amesema kuwa ameonyesha kwa hali na mali alikuwa na mali ila mkarimu na amefanya mengi ya heshima kubwa,alijitoa bila kujali alipanda miti zaidi ya milioni ishirini siyo jambo la kawaida.

"Nawaomba wananchi wenzangu msiamini kila kitu kinachoandikwa  kwenye mitandao ya kijamii ,vingine vya  uongo sana.amesema Ndugai

Kwa zaidi ya mzee mwenzangu ameshatangulia mbele za haki haitajalisha tutazungumza maneno mazuri kiasi gani ,tutakachowezakukifanya sasa ni kuyaishia kuyaenzi mema aliyotenda,alikuwa mnyenyekevu,kauli zake zilikuwa za kujenga,kupatanisha,mamlaka,fedha zinajenga kiburi zisipotumika vizuri,hakuwa kiongozi wa serikali .

 Dkt. Mengi amezikwa  katika kijiji cha Kisereni Machame mkoani Kilimanjaro, eneo la makaburi ya familia walipozikwa wazazi wake na ndugu wengi.
TIZAMA HAPA PICHA ZOTE KATIKA TUKIO HILO KUANZIA WAZIRI MKUU    AKIPOKELEWA KATIKA UWANJA WA NDEGE WA KIMATAIFA KIA AIRPOT.
  


 




























Hakuna maoni:

Chapisha Maoni