| Hiki ni kikosi cha Polisi Tanzania Fc wakiongozwa na Captain Henerico. |
Timu ya
Polisi Tanzania imeibuka kidedea na kufuzu kushiriki ligi kuu daraja la
kwanza Tanzania bara mara baada ya
kuitandika Bora Fc bao 2-1.
Kikosi
cha Polisi Tanzania kikiwa chini ya Captain Henerico Kayombo wameweza
kujichukulia pointi tatu kibindoni na kuifanya safari kuwa nyepesi ya kuelekea ligi kuu Tanzania bara hapo badae.
Mabao
hayo yamefungwa namchezaji nguli jezi
nambari 4 mgongoni Patrick Athanas na
kuwainua mashabiki katika viti kwa kukonga nyoyo zao huku ushangiliaji wa aina yake ukishika hatamu.
Kikosi
hicho cha Polisi Fc kiliongozwa na wachezaji
Abdulikarim Segeja,Kurwa
Manzi,Mohamed Kassim,Patrick Athanas,Hassan Kapona,Henerico Kayombo ,Bantu
Admin,Juma Ramadhan,Charles Ndahaze,Santos Marcelino na Shaban Stambuli.
Akizungumza
mara baada ya mchezo huo Afisa habari wa timu hiyo Bw.Frank Geofray amesema
ushindi huo ni sehemu muhimu kwao na kati ya mafanikio yanayosadifu umuhimu wa
timu hiyo kwani walikua wanatambua wanachokifanya sambamba na kushukuru uongozi
mzima wa timu hiyo katika kuwawezesha kwa hali na mali kuyafikia mafanikio
hayo.
HAPA NI KABLA YA MCHEZO MAANDALIZI NA MORALI ZINAONEKANA ZAIDI KWA WACHEZAJI NA MASHABIKI.
| Hawa ndio Boma Fc ya Mbeya. |
| Kamanda wa Polisi Mkoa wa Kilimanjaro Hamis Issa akiwa amewasili kabla ya mechi kuanza ili kushuhudia mtanange huo. |
| Mkuu wa Mkoa Kilimanjaro Dkt.Anna Mgwhira akiwa tayari kufuatilia mechi hiyo. |
TIZAMA HAPA MKUU WA MKOA WA KILIMANJARO DR.ANNA MGWHIRA AKISALIMIANA NA WACHEZAJI KABLA YA MECHI HIYO KUANZA.
HAYA NDIO MAGOLI YA POLISITANZANIA FC DHIDI YA BOMA FC YA MBEYA.
| Patrick Athanas anafunga bao la pili na kuwainua mashabiki wa Polisi Tanzania kwenye Majukwaa. |
| Kamanda wa Polisi Hamisi Issa akiwa na Furaha mara baada ya Polisi Tanzania Fc kupata bao la pili. |
| Mkuu wa Mkoa wa Kilimanjaro Dr.Anna Mgwhira akifuatilia kwa makini mtanange huo. |
| Kamanda Issa akishauriana jambo na Mkuu wa Mkoa wa Kilimanjaro mwisho kabisa upande wa kushoto ni Kaimu Katibu Tawala mkoa wa Kilimanjaro Bw. Bwai Biseko . |
| Kamanda Issa akishauriana jambo na Mkuu wa Mkoa wa Kilimanjaro mwisho kabisa upande wa kushoto ni Kaimu Katibu Tawala mkoa wa Kilimanjaro Bw. Bwai Biseko . |
| Kamanda Issa akishauriana jambo na Mkuu wa Mkoa wa Kilimanjaro mwisho kabisa upande wa kushoto ni Kaimu Katibu Tawala mkoa wa Kilimanjaro Bw. Bwai Biseko . |
| Dr.Mgwhira akistaajabu jambo la kimichezo mara baada ya kupata ufafanuzi kutoka kwa Katibu Tawala wa mkoa Bw.Bwai Biseko. |
| Picha zifuatazo ni Kocha kiongozi wa timu ya Polisi Tanzania Pamoja na jopo lake akitoa maelekezo kwa wachezaji wake mara baada ya kipindi cha kwanza kukamilika. |
| Mlinda mlango wa timu ya Polisi Tanzania Fc Abdulkarim Segeja akijizatiti kukamilisha Ng'we ya pili katika chezo huo. |
| Wachezaji wakijizatiti kuukabili mpira katika kipindi cha pili. |
| Mmoja wa washabiki wa timu ya Polisi Tanzania Fc Akishangilia na kujipongeza mara tu ya Refarii kupuliza kipenga cha Mwisho. |