![](https://blogger.googleusercontent.com/img/b/R29vZ2xl/AVvXsEj5n7Dvcjh-nA7IuFileO-YPAZyG7q57_dbD9unmjflQzReyfwRA5jYIG3RY0IB8CQ-r_ulUvipmPqEsb8buLEkb0MuNib2fHlShJNdeh43ixR2GN9LnQrAWlEA_4nMF8oqEogqEE1W8piR/s640/PMO_2736%25284%2529.JPG) |
Waziri Mkuu, Kassim Majaliwa akizindua Shule ya Sekondari ya ST.
Pamachius Inclusive iliyopo katika kijiji cha Kimashuku wilayani Hai,
Februari 22, 2019. Kulia ni Mke wa Waziri Mkuu, Mama Mary Majaliwa na wa
pili kulia ni Askofu Mkuu wa Jimbo Kuu la Arusha, Mhashamu Isaac Amani,
kushoto ni Mkuu wa mkoa wa Kilimanjaro, Anna Mgwira na wa pili kushoto
ni Waziri wa Elimu, Sayansi na Tekinolojia, Profesa Joyce Ndalichako. |
Waziri mkuu wa Jamhuri
ya Muungano wa Tanzania mhe. Kassim Majaliwa ametoa wito kwa wakuu wa Wilaya
hapa nchini kushirikiana na wazazi
katika kuhakikisha wanawafichua watoto wenye ulemavu kwa lengo la kuwapatia
elimu.
Ametoa wito huo mkoani
Kilimanjaro katika ziara yake mkoani humo hii leo wakati akizungumza katika
uzinduzi wa shule jumuishi ya secondari St. Pamachius Inclusive iliyopo katika kata ya
Mnadani kijiji cha Kimashuku wilayani Hai.
Amesema Serikali
imeendelea kutoa kipaumbele kwa watu wenye ulemavu wa aina tofautitofauti kwa kutenga bajeti zenye tija ikiwemo kuendeleza
miundombinu wezeshi katika Chuo cha
ualimu Patandi ambapo mradi huo umegharimu
zaidi ya shilingi billion 2 za
kitanzania .
Akifafanua zaidi
Majaliwa amezitaka taasisi mbalimbali za dini na watu binafsi kujikita zaidi
katika kuchangia ujenzi wa miundo mbinu wezeshi ,huduma za afya na mahitaji
muhimu yanayotegemewa na makundi mbalimbali yenye uhitaji katika taifa ambapo amempongeza Dkt.Reginald Mengi kwa kuwa
mzalendo wa kwanza kuchangia huduma mbalimbali.
Kwa upande wake
mwalimu mkuu wa shule hiyo Padre Patrick Asanterabi amesema shule hiyo ilianza
ujenzi wake tangu mwaka 2015 na kuanza kutoa elimu kwa wanafunzi wa kidato cha
Kwanza January 5 mwaka huu ambayo hadi sasa inawanafunzi 74, 34 wasichana na 40
waluvana.
Katika hatua hiyo
Asanterabi ameishukuru Serikali na wadau wa elimu kwa mchango wao wa hali na
mali katika kuhakikisha shule hiyo inayojumuisha wanafunzi wenye ulemavu na
wanafunziwa kawaida na kufikia malengo
yaliyokududiwa na Askofu mkuu jimbo la Arusha Isaac Amani.
TIZAMA PICHA MUHIMU HAPA KATIKA UZINDUZI HUO.
![](https://blogger.googleusercontent.com/img/b/R29vZ2xl/AVvXsEj8QAZJzCaQATZEYrj-OcKkO5-oaXNVZ2rfgNiYdrZsgXOl99moHB-wiVemNsL_oNT0ZpQKok9hOzGZrbSW_R9hNi56mBiU29rYX8o8OLqc6N7gwBE9Lo2LrPUB8KUBO8pTL-f-PMzbCpN9/s640/PMO_2684.JPG) |
Waziri Mkuu, Kassim Majaliwa akisalimiana na Askofu Mkuu wa Jimbo Kuu la
Arusha, Mhashamu Isaac Amani wakati alipowasili kwenye viwanja vya
Shule ya Sekondari ya ST. Pamachius Inclusive iliyopo katika kijiji cha
Kimashuku wilayani Hai kuzindua shule hiyo, Februari 22, 2019. Katikati
ni Mke wa Waziri Mkuu, Mama Mary Majaliwa. | |
![](https://blogger.googleusercontent.com/img/b/R29vZ2xl/AVvXsEgbpaljg4kIub3Y2_PrdEGSEyJKlLQm7jLElBB_fyVnlzNHInK8miGuRU3OHga96bSYJ_hL5WPdcNXSe5m08rMYLRggJ92ACUGvmLvkHxb04wChduc91XKlEtwErlFWJsQ588o1_0TczHQ_/s640/PMO_2706.JPG) |
Mke wa Waziri Mkuu, Mama Mary Majaliwa akizungumza na Mkuu wa Mkoa wa
Kilimanjaro, Anna Mgwira katika uzinduzi wa Shule ya Sekondari ya ST.
Pamachius Inclusive iliyoyopo katika kijiji cha Kimashuku wilayani Hai
uliofanywa na Waziri Mkuu, Kassim Majaliwa Februari 22, 2019. |
![](https://blogger.googleusercontent.com/img/b/R29vZ2xl/AVvXsEiSGzxyCskXmOjtAWM9GVfxhw8A7HLkPO650ji6c680QBug74-CWUYEwJGvm9G7xceSM4-HsiQpfJEIHoblPZqoEGwmbgOsHoHbLu2OAPcc6DkpANO8JI_d503ezkIYLnLgc2dP0t9FaPSL/s640/PMO_2690.JPG) |
Waziri Mkuu, Kassim Majaliwa akisalimiana na Mwenyekiti Mtendaji wa
Makampuni ya IPP, Dkt. Reginald Mengi wakati alipowasili kwenye Shule
ya Sekondari ya ST. Pamachius Inclusive iliyopo katika kijiji cha
Kimashuku wilayani Hai kuzindua shule hiyo, Februari 22, 2019. | | | | | |
![](https://blogger.googleusercontent.com/img/b/R29vZ2xl/AVvXsEijaA1oweoIAYaAD0BRedYKQuF7XFAiw2zP8IRpGzr3rysFCT8LR5kBVyVh1UdiU7egVPH0GMnF7XPk6457LHSrZrMQuKLM_UZChyphenhyphenVXUdyTX8LJjJoYQVJArCbNgnqShJbLxXJMe_y1_Xxu/s640/PMO_2707.JPG) |
Waziri Mkuu, Kassim Majaliwa akitia saini kitabu cha wageni wakati
alipowasili kwenye Shule ya Sekondari ya ST. Pamachius Inclusive
iliyopo katika kijiji cha Kimashuku wilayani Hai kabla ya kuzindua
Shule hiyo, Februari 22, 2019. Kulia ni Askofu Mkuu wa Jimbo Kuu la
Arusha, Mhashamu Isaac Amani. | | |
![](https://blogger.googleusercontent.com/img/b/R29vZ2xl/AVvXsEiDOI9iwoMWNTztza0DG_xXeiw99zkoZFW77W9VTQunaXengWBqVD4m5-xfwc6o2660VTsjts8ruJnVS0-9v7srDxlbj6hIPK9B6xslUAKUAckM0hltGKSXRGirXKaYAzOp31P9by7ttEbQ/s640/PMO_2733.JPG) |
Waziri Mkuu, Kassim Majaliwa akizindua Shule ya Sekondari ya ST.
Pamachius Inclusive iliyopo katika kijiji cha Kimashuku wilayani Hai,
Februari 22, 2019. Kulia ni Mke wa Waziri Mkuu, Mama Mary Majaliwa na wa
pili kulia ni Askofu Mkuu wa Jimbo Kuu la Arusha, Mhashamu Isaac Amani,
kushoto ni Mkuu wa mkoa wa Kilimanjaro, Anna Mgwira na wa pili kushoto
ni Waziri wa Elimu, Sayansi na Tekinolojia, Profesa Joyce Ndalichako. |
![](https://blogger.googleusercontent.com/img/b/R29vZ2xl/AVvXsEiq6l6xcflrQO-VE5fB4sAG84gIGriLGNuupWvyuwXF8URnwLcxrHdmDxJBOMHYSiVyOW0NIOzPlUzFX0KtyMpyXK2MXPOwQF-6s-MWIOGcd-OPXiZ1ZhepcrQa_X4QlK9jtGSYGDz8Z1EE/s640/PMO_2813.JPG) |
Waziri Mkuu, Kassim Majaliwa na mkewe, Mary wakikagua madawati kwenye
moja ya madarasa ya Shule ya Seondari ya ST. Pamachius Inclusive
iliyopo katika kijiji cha Kimashuku wilayani Hai, iliyozinduliwa na
Waziri Mkuu, Februari 22, 2019. Kushoto ni Askofu Mkuu wa Jimbo Kuu la
Arusha, Mhashamu Isaac Amani na kulia ni Waziri wa Elimu, Sayansi na
Tekinolojia, Joyce Ndalichako. |
![](https://blogger.googleusercontent.com/img/b/R29vZ2xl/AVvXsEjuGhy0SfCzhnNhXW3buNx3BpmW5s1X8ZfR82zMPecd3EhxbZbC6JE0h2bMVtJTnL1u79Zmah7nPcnWLUOp3u2MKbqdiT9_li6RUjgNTckj0xVM6yNhoeYMk5on71x7DvbmlmpMz6thkAXE/s640/PMO_2827.JPG) |
Waziri Mkuu, Kassim Majaliwa akiwa amekaa kwenye dawati wakati
alipokagua madrasa ya Shule ya Sekondari ya ST. Pamachius Inclusive
iliyopo katika kijiji cha Kimashuku wilayani Hai baada ya kuizindua
Shule hiyo, Februari 22, 2019. Wengine kutoka kushoto ni Mke wa Waziri
Mkuu, Mama Mary Majaliwa, Askofu Mkuu wa Jimbo Kuu la Arusha, Mhashamu
Isaack Amani, Waziri wa Elimu, Sayansi na Tekinolojia, Profesa Joyce
Nadlichako na kulia ni Mkuu wa Mkoa wa Kilimanjaro, Anna Mgwira. |
![](https://blogger.googleusercontent.com/img/b/R29vZ2xl/AVvXsEg0Hj794cTcjN93GZdeFDf5mp1nLdfhcpvubdb-V_MAhQS_0ZirvqXZDGfX-R1URu5Eyg6PxSViUFy0ebR0tu8klkrBBxc3OUjculrbBBqb8nToRarmdogPfpdOpLLaUzDs3J_doFEw8uF7/s640/PMO_2842.JPG) |
Wananchi wakimsikiliza Waziri Mkuu, Kassim Majaliwa wakati
alipozungumza baada kuzindua Shule ya Sekondari ya ST. Pamachius
Inclusive katika kijiji cha Kimashuku wilayani Hai, Februari 22, 2019. |
![](https://blogger.googleusercontent.com/img/b/R29vZ2xl/AVvXsEgosmsmV6vfhsFCSqaqiTD5hW-YS9qH6VWNjxtd7K4AMYMgBXIgjE7R5iRKQFQh178awbi9DZNuBnW5nvmqPL49w78n01dEQAp1WV2rcLquOD7xQA3Fw-YMe-RuNuRIbzudJRaCtzXSvsp8/s640/SAM_0122.JPG) |
Wananchi wakimsikiliza Waziri Mkuu, Kassim Majaliwa wakati
alipozungumza baada kuzindua Shule ya Sekondari ya ST. Pamachius
Inclusive katika kijiji cha Kimashuku wilayani Hai, Februari 22, 2019. |
![](https://blogger.googleusercontent.com/img/b/R29vZ2xl/AVvXsEieebBqR1UFm8ksqUJm5N0OH6VacCfvUP5SAVV_lS14CWEtKR2W_zm1ksCfnUWAA77OVBcvmxUDtSpoIvv8MHEFTyq8-fn7rH8qV9uwaKswlwrx449hXTweky3gH1sNrXm3jEl5_y6CwqhX/s640/SAM_0092.JPG) |
Baadhi ya wanafunzi weye uhitaji maalum katika Shule ya Sekondari ya ST. Pamachius
Inclusive katika kijiji cha Kimashuku wilayani Hai, Februari 22, 2019. |
![](https://blogger.googleusercontent.com/img/b/R29vZ2xl/AVvXsEhhQf3-xRC7POYS5Q2W_cA7iO0grqtbANPfyQp_La9uyCEmtEHXY98OKL4PwbNUNhWn9QGBS2v7mZvlHLnl2_snqeYgDyIwKCi7pFhQ3fEudyN61S9Z_pyNhH9VtAd1-lFYzG1Diq5CtIjd/s640/SAM_0159.JPG) |
Waziri Mkuu, Kassim Majaliwa wakati
akishuhudua mwanafunzi Joseph Mtei ambaye hana mikono yote miwili akiandika kwa kutumia vidole vya miguu baada kuzindua Shule ya Sekondari ya ST. Pamachius
Inclusive katika kijiji cha Kimashuku wilayani Hai, Februari 22, 2019.![](https://blogger.googleusercontent.com/img/b/R29vZ2xl/AVvXsEg0Jw6fbS-_3O95vMQQSXyA79UbNeRISFNk21ayi4-bJEx8O3lS6TkCjX632VauedNGoQNNkqlXBxH6bcrxH7TKTK_AfZpBmKmJ-dw5lJFTg2Mg54908xOsFUKIbvN9IPXnAio680fWvuI_/s640/SAM_0168.JPG) |
![](https://blogger.googleusercontent.com/img/b/R29vZ2xl/AVvXsEgJ7F3oRCyhAdbQ52NlhqB1xBZIda7Nln_gTBWEn8qYWj9iwfwnhfHwVfQf_-Boh2xkLiJc0H2k_uYGi3_fzJ6tXqlA-ylx1Y9wbZYCo6XCLPr-ABCYd1eDnTEfqxr3W3OOu7HaU_lfEobz/s640/SAM_0115.JPG)
Moja ya Darasa katika Shule ya Sekondari ya ST. Pamachius
Inclusive katika kijiji cha Kimashuku wilayani Hai, Waziri Mkuu, Kassim Majaliwa wakati
alipozungumza baada kuzindua Februari 22, 2019.
![](https://blogger.googleusercontent.com/img/b/R29vZ2xl/AVvXsEjuxTFJk98mL5lrWZnkil0JvBn4I3MdhwJAjphb4Bka8oVK72aG5u4LXtiogayeCjhOzOG4IM1fbkCCo9rUOSqNZX54Lm36Q_ZQ1uhA-XfneGk5VMr3X3kAg9sE43KZfTNrIQB_BfIsb3h7/s640/SAM_0132.JPG) |
Wanafunzi wa Shule ya Sekondari ya ST. Pamachius
Inclusive katika kijiji cha Kimashuku wilayani Hai,wakitoa salaam kwa mgeni rasmi Waziri Mkuu, Kassim Majaliwa , Februari 22, 2019.
|
Hakuna maoni:
Chapisha Maoni