Tafuta katika Blogu Hii

Jumamosi, 23 Februari 2019

MAJILIWA AKABIDHI RUNGU KWA VYOMBO VYA DOLA ,AWAGEUKIA WATUMISHI WA UMMA NA WATENGEZAJI WA POMBE HARAMU

Waziri Mkuu waJamhuri ya Muungano wa Tanzania , Kassim Majaliwa akivisisitiza vyombo vya usala kuhusu ulinzi katika mpaka wa holili.

Waziri mkuu wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe.Kassim Majaliwa ameviagiza vyombo vya dola kuimarisha ulinzi wa kutosha katika mpaka wa Holili na kizisisitiza Mamlaka zinazohusika kutimiza wajibu huo  kufuata sheria,kanuni na taratibu zilizowekwa na serikali.  

Akizungumza katika ziara yake ya kikazi katika  kituo cha Forodha Holili, wilayani Rombo Majaliwa amesema serikali inatambua umuhimu wa mipaka iliyopo wilayani humo  sambamba na michango muhimu katika kuhakikisha  fursa muhimu za kijamii zinafikiwa na kuleta tija kwa wananchi.

Akifafanua zaidi amewataka wananchi wanaofanya shughuli za kukuza uchumi hususani katika sekta ya biashara ndani na nje ya mipaka  ya Tanzania na Nchi jirani kufuata taratibu zilizowekwa na Serikali  ili kuimarisha na kuendeleza hali ya amani na utulivu .

” Katika kukuza uchumi wa taifa Serikali ina kila sababu ya kusimamia na kulinda mipaka yake hapa nchini sambamba na  kuhakikisha wananchi wanapata huduma stahiki kupitia sekta mbalimbali za kijamii na kiuchumi hivyo nawataka watumishi wa umma kushirikiana na wananchi kuwafichua wale wote wanaojihusisha na biashara za magendo zinazosababisha serikali kukosa mapato  pamoja na kuthibiti mianya ya rushwa ”. Alisema Majaliwa.

Katika hatua hiyo Majaliwa amewataka wakuu wa Idara  hapa nchini kushirikiana na watendaji wa serikali kupokea  na kutoa ushauri  wa kitaalaam katika kutekeleza wajibu wao kwa wakati na kuhakikisha changamoto mbalimbali za wananchi zinatatuliwa na kuibua fursa zitakazochangia ongezeko la ajira kwa wazawa  .

“Serikali ya awamu ya tano ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania itaendelea kuchukua hatua  stahiki kwa mtumishi yeyote yule Mvivu,Mla rushwa ,Mwizi,Mbadhilifu na Mzembe hivyo simamieni vizuri vyanzo vya mapato na rasilimali muhimu katika ustawi wa uchumi”Alisema Majaliwa.

Akizungumzia kuhusiana na swala la Pombe haramu zaidi ya 48 zinazotengenezwa wilayani humo  ameziagiza kamati  ya ulinzi na usalama kufanya msako mkali haraka iwezekanavyo katika kubaini mitambo yote inayotumika na wahusika kuchukuliwa hatua kali za kisheria .
“Awamu ya tano haipo tayari kuona wananchi wake wanadhohofika afya zao kutokana na matumizi mabaya yanayotokana na unywaji wa pombe ,tumedhamiria kuwahudumia wananchi katika sekta mbalimbali ikiwemo elimu na afya hivyo sina budi kusema vyombo vya dola kamata ,weka ndani, chunguza na wapelekeni Mahakamani”Alisema…..
            TIZAMA PICHA HIZI JINSI MAJALIWA ALIVYOKABIDHIWA ZAWADI  HII.
Waziri Mkuu, Kassim Majaliwa na Mkewe Mary wakifuhia picha  waliyozawadiwa na mchoraji maarufu wilayani Rombo,  Yusti Oiso  (kushoto)  wakati alipozungungumza na watumishi wa Halmashauri ya wilaya ya Rombo kwenye ukumbi wa Shule ya Sekondari ya Shauritanga wilayani humo, Februari 23, 2019.
Waziri Mkuu, Kassim Majaliwa akipokea  picha  aliyozawadiwa na mchoraji maarufu wilayani Rombo,  Yusti Oiso  (kushoto)  wakati alipozungungumza na watumishi wa Halmashauri ya wilaya ya Rombo kwenye ukumbi wa Shule ya Sekondari ya Shauritanga wilayani humo, Februari 23, 2019.

Hakuna maoni:

Chapisha Maoni