Msiwaone
wamebeba mabegi mkazani ni wasafiri au wanafunzi mitihani yao ni kupenya katika
viunga mbalimbali vya miji kutimiza azima zao.
Kwa miaka
mingi hivi sasa biashara ya madawa ya kulevya imekua ikishamiri siku hadi siku
kama biashara nyingine zinazofanywa na wajasiriamali tofatoutitofauti na
kusababisha madhara mbalimbali kwa
watumiaji ,wanajamii , taifa la leo na la kesho licha ya kuwepo kwa sheria ya
mwaka 2015 kifungu namba 5 inayopinga matumizi na biashara hii haramu.
Mbali na
kuwepo kauli mbiu inayosadifu mwenendo utakaokuza uchumi wa kati na sera ya
taifa la Tanzania “HAPA KAZI TU”serikali lazima ichukukue hatua thabiti
yakukomesha na kutokomeza aina mbalimbali za madawa ya kulevya yanayopatikana
hapa nchini ikiwemo bangi,kokeini,miadarati na nyinginezo.
Sina budi
kusema serikali yaani mimi ,wewe na viongozi mbalimbali tuliowapa dhamana ya
kutuongoza bila kuwasahau wazalendo wote
wenye mapenzi mema na taifa lao
haijalishi ni mjini au vijini kwani waswahili husema “maji ukishayavulia nguo
sharti uyaoge” halikadhalika “Tembo hashindwi na mkonga wake” kwa mantiki hii tukishirikiana kwa pamoja tunaweza kufikia
malengo ya kukomesha na kutokomeza kabisa matumizi ya madawa ya kulevya.
Mashirika mbalimbali
na taasisi za kidini zimekua zikipambana vilivyo kuwaelimisha waumini wa kada
mbalimbali kupitia mahubiri na makongamano juu ya hathari zinazopatikana na
matumizi hayo huku ushirikiano hafifu katika kuwabaini wahusika kutoka kwa
wananchi, mamlaka husika zilizopewa dhamana ya kushughulikia maswala
haya nyeti na baadhi ya viongozi
tuliowapa ridhaa ya kutuongoza wakituhumiwa kuwa wanachangia kwa kiasi kikubwa kuendeleza
biashara hii haramu kwa mantiki ya kupalilia na kulinda kura na nyanzifa zao katika kipindi kijacho.
Hii ni
dhairi kwamba viongozi hawa wanawafahamu fika baadhi ya wafanya biashara hao katika maeneo yao na
kama sio kuwafahamu fika, wanatambua uwepo wa biashara hizi katika maeneo mbalimbali wanayoyasimamia katika
shughuli zao za kiutawala.
Vimekuepo
viashiria mbalimbali vya upatikanaji wa madawa hayo ya kulevya kama uwepo wa
viatu juu ya nyaya za nguzo za
umeme,mifuniko ya ndoo na kadhalika huku ushindani wa soko ukisimamiwa na wananchi wa tabaka la chini.
Nchini
Tanzania baadhi ya viongozi wamekua wanatumia fulsa hii kwa wananchi kama mtaji
wao wa kisiasa katika kampeni mbalimbali wakiwa na lugha iliosheheni ladha
nzuri ya sera na mikakati ya kimaendeleo katika miundombinu mbalimbali ikiwemo Afya ,Elimu nk. lakini sio kupunguza na hatimaye
kutokomeza kabisa biashara hizi haramu.
Ukipita
katikati ya miji utaliona taifa la leo likiwa limegubikwa na ulevi wa madawa
hayo,utayaona na hata kukutana na makundi mbalimbali ya watumiaji na waathiriwa
wa dawa hizo wakijaribu kupambambana kwa kila hali kupata chochote wakijidai
wapiga debe na wabeba mizigo ndani ya miavuli iliyosheheni maasi mbalimbali
ikiwemo udokozi,wizi,ubakaji na hata ulawiti.
Sauti zao
zinasikika katika ladha tofautitofauti zikiwa zimebeba fikra chanya za
uwajibikaji “mia tano mpaka nitakapoufikisha mzigo” kauli hii inachukua hatamu
“mjini hakuna mashamba karibu tuwajibike hatuwezi kulima lami”hapo inakubidi
uwe makini kuchunga vile ulivyo navyo haijalishi ni mkate,simu ya
mkoni,fedha,pochi au chochote ulichobeba kama zawadi huko uendapo.
Swali la
kuweza kujiuliza je?katika maeneo hayo ni kwamba hakuna uongozi au viongozi hao
ni vipofu wa fikra au wapo katika miavuli ya kulinda kura zao kupitia chaguzi
mbalimbali.
Jibu la haraka
linaweza kupatikana katika fikra hii “bora liende matumizi ya kwao ,waathirika wao kura za kwangu”
na kuibua sura yenye taswira tofauti kwa viongozi wateule wa Mh.Rais kuwa
wana viburi hawafai kuwa viongozi na kufikia hata hatua ya udhalilishaji na kuingiliwa
faragha zao.
Ili
kuendana na kasi ya Mh.Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania John Magufuli “Tanzania
ya viwanda”ni vyema wateule wa rais kuunda jukwaa la pamoja na
kuungana kwa pamoja katika kukomesha biashara haramu kwa kushirikiana na vyombo
vya dola ambapo kimsingi vyombo hivyo wanadhamana kubwa ya kulinda rasilimali mali na
watu kwani wao ni Wenyeviti wa kamati za ulinzi na
usalama.
Ninaposema
rasilimali watu ninamaanisha kwa dhati kabisa viwanda bila nguvu kazi watu ni
kazi bure kutokana na athari mbalimbali zinazowakuta walengwa ikiwemo sababu za
kiafya na kiuchumi.
Hii ni
dhairi kwamba waraibu wengi wa dawa za kulevya wanaopatikana mtaani
niwaaathirika wa virusi vya ukimwi (VVU)asilimia kubwa wamekua wakijikatia tamaa
huku wauzaji wakijipatia faida kedekede “wanaishi vizuri ,wanamiliki vitega uchumi
vya gharama kubwa ikiwemo magari ya kifahari na majumba”.
Mimi
nafikiri mkono mrefu wa serikali ungeanza kuwakamata na kuwachukuli hatua stahiki
tungeweza kumaliza tatizo hili kabisa, mawakala na wasambazaji wa dawa hizi za
kulevya ndio chazo cha kushamiri kwa biashara hii hivyo,wakiwaunganishwa na watumiaji kunaweza kupatikana suluhu na kuifanya
Tanzania ya Viwanda na bila madawa inawezekana kwani wote hawa jamii inawatambua.
Mchambuzi wa
makala hii anaweza kuwa na mwarobaini sahihi wa tatizo hili kama haki itatendeka
kwa usawa na sio kununuliwa inasikitisha kabisa kuona biashara hii inafanyika
kwa uwazi kabisa kama biashara halali”wauzaji na wasambazaji wamekua kama wamachinga
katikati ya mji na baadhi ya watumishi wa vyombo vya dola wakishindwa kutimiza wajibu wanawakamata sasa hivi baada ya muda wamewaachia kwa mantiki hii baadhi yao wamekua
kama watoza ushuru“je? tupo salama!
Kumekuwepo
na viongozi wenye ujasiri na utashi mkubwa wakudhibiti maovu kwa kauli mbiu
mbalimbali kama “watapata tabu sana,Dar es salaam salama”na kadhalika huku wakiibua
hisia zenye tija kwa baadhi ya watanzania wenye nia salama na nchi yao hii
inaonyesha dhahiri kwamba Mh.Rais ana nia njema yakuifikisha Tanzania mbali
kiuchumi “HAPA KAZI TU.”
Mchambuzi wa
makala hii hana budi kusema huenda chanzo cha kushamiri kwa biashara ya madawa
ya kulevya nchini Tanzania inatokana na kutokuwepo kwa viongozi wasio wazalendo
na uwepo wa baadhi ya nchi jirani kuhalalisha matumizi ya madawa ya kulevya kama
moja ya starehe na faragha ya mtu hivyo kurahisisha upatikanaji huo na kuleta
taswira yenye uhalisia wa biashara hiyo kuanzia mipakani mwa nchi hizo kuelekea
vijijini ,mjini,kata,tarafa, wilaya,mkoa na hatimaye nchi nzima hivyo kuitaka
serikali kutizama swala hili kwa jicho la tatu na kuleta fikra mpya.