Tafuta katika Blogu Hii

Jumanne, 22 Agosti 2017

JAFARY MICHAEL AMALIZA UTATA JIMBONI KWAKE ABAINISHA MBIVU NA MBICHI AJIKITA KUPIGANIA HAKI NA WAJIBU KWA MAENDELEO YA UCHUMI WA JIMBO LA MOSHI MJINI.



MBUNGE WA MOSHI MJINI JAFARY MICHAEL AKIWAHUTUBIA WANANCHI WALIOKUSANYIKA KATIKA MKUTANO WA ADHARA KATIKA VIUNGA VYA KIBOROLONI.

Mbunge wa jimbo la Moshi mjini Jafari Michael amesema ni vyema jamii ikatambua mchango mkubwa unaotolewa na viongozi pasipo kuangalia itikadi za vyama vya siasa na kukubali kukosolewa pindi wanapokosea ili kujenga fursa ya usawa na kuharakisha shughuli za maendeleo.
Akizungumza katika mkutano wa adhara uliofanyika katika kata ya Kiboroloni na kujumuisha viongozi mbalimbali wa umma Michael amekanusha kumekuwepo na kauli za kisiasa zinazowapotosha wananchi katika shughuli za kukuza uchumi ikiwemo katazo la biashara ya mitumba kuendelea katika soko la  Kiboroloni na kuathiri soko kuu la mitumba Memorial ni uwongo mtupu.
Hata hivyo amesema kauli  hizo zinalishusha hadhi soko hilo kwa kulitangaza kuwa limekufa  hali inayochangia kudorora kwa uchumi kwa wafanyabiashara wadogowadogo alimaarufu kama machinga na kuwapunguzia dhana ya uwajibikaji na kuwakatisha tamaa baadhi yao kutafuta maslahi yao kwa manufaa ya kukuza uchumi na kuboresha maisha yao hali inayopelekea kuzorota kwa shughuli mbalimbali, ukiukwaji wa haki na kunyanyasika kwa baadhi ya wajasiriamali pasipo tija.
Akifafanua zaidi Michael amesema dhamira kuu ya Chama cha Demokrasia na Maendeleo(CHADEMA)katika jimbo la Moshi mjini ni kupanua wigo wa uchumi kwa kushughulikia vikwazo mbalimbali  vinavyochangia kukwamisha na kukuza uchumi sambamba na kutatua matatizo yanayowakabili wananchi kupitia sekta mbalimbali ikiwemo upungufu wa ajira unaosababishwa na kufa kwa viwanda mbalimbali na upungufu wa  miundombinu thabiti unaopelekea kuzorota kwa shughuli za maendeleo ya jamii.
Akizungumzia swala la miundombinu ni pamoja na kufa kwa reli ya TAZARA iliyokua ikitumika kutoka Tanga,Moshi,Arusha mpaka Musoma ambapo ameshafanya majadiliano na waziri mwenye dhamana pamoja na mkurugenzi mkuu wa shirika la reli Tanzania kupitia bunge la bajeti na kamati ya miundombinu ambapo yeye akiwa kama mjumbe wameafiki  kushughulikia kuikarabati reli hiyo kwa kutenga fedha itakavyowezekana na hatimaye reli hiyo kuanza kutumika kusafirisha mizigo huku mchakato wa ujenzi wa kisasa ukiendelea hapo baadae.  

Akivitaja baadhi ya viwanda hivyo ni pamoja na Magunia ,Madawa  na Kibo Match ambapo amesema amekua akijitahidi kwa kiasi kikubwa kujenga hoja mara kwa mara bungeni na kuishawishi serikali kuu kuhusu umuhimu wa viwanda hivyo na faida mbalimbali  zitakazopatikana na hatimaye waziri mwenye dhamana ameahidi kushughulikia swala hilo mara moja na kuwataka wananchi wa Moshi kujiandaa rasmini katika fursa za ajira kupitia sekta ya viwanda. 
HAWA NI BAADHI YA WANANCHI WAKIMSIKILIZA MBUNGE WAO KWA SHAUKU KUBWA YA KUFAHAMU MAMBO MBALIMBALI . 
PAKUA SAUTI VIDEO NA PICHA BAADA YA MUDA MFUPI KUHUSU MKUTANO HUO BILA KUKOSA .

Hakuna maoni:

Chapisha Maoni