Tafuta katika Blogu Hii

Jumatano, 6 Septemba 2017

ANNA MGHWIRA AFANYA ZIARA KATIKA WILAYA YA ROMBO NA MARANGU AHIMIZA UHIFADHI ZAIDI WA RASILIMALI ZA TAIFA AWAUNGA MKONO TANAPA KUPITIA UJIRANI MWEMA .

 Katika picha ni Muikolojia wa Hifadhi ya Taifa ya Kilimanjaro (KINAPA) Bw.Imani Kikoti  akiwa ameambatana na  Mkuuu wa Mkoa wa Kilimanjaro Mhe.Anna  Mghwira  na kulia ni Afisa misitu mkoa wa kilimanjaro Bw.Emmanuel Kyengi.

Mkuu wa mkoa wa Kilimanjaro bi.Anna Mghwira amewataka wananchi waishio pembezoni mwa hifadhi za taifa ya Kilimanjaro (KINAPA)kuwa waaminifu na waadilifu sambamba na kutumia fursa ya kulinda na kuhifadhi mazingira ili kuboresha soko la utalii litakalochangia ongezeko la ajira na kuwanufaisha watanzania kiuchumi.
Akizungumza katika ziara ya kushitukiza katika wilaya ya Rombo na Marangu Mghwira amesema njia pekee ya kujenga mahusiano na ujirani mwema baina ya wananchi na shirika la uhifadhi KINAPA ni ushirikiswaji wa mambo muhimu yanayotarajiwa kufanyika sambamba na kutoa taarifa kwa wakati juu ya vitendo viovu vinavyofanywa na baadhi ya wananchi kinyume na utaratibu wa sheria.
Mgwhira  amesema anatambua jitihada za hali na mali  zinazofanywa na wadau hao wa  maendeleo kwa kuiunga mkono serikali katika kutambua umuhimu wa uhifadhi ambao ni pamoja na kuhakikisha mandhari na aina mbalimbali ya uoto wa asili unahifadhiwa ikiwemo uhifadhi wa wanyamapori kwa ajili ya Utalii, kuhifadhi wanyama wanaotishiwa kutoweka kama vile Sokwe, Tembo na Faru.

Baadhi ya wananchi wa Kijiji cha  Ubetu ambacho ni moja ya vijiji vinavyopakana na hifadhi hiyo wilayani Rombo wamesema kumekua na unyanyaswaji wa wanawake  ndani ya hifadhi hiyo kila kuchwapo.
 Akifafanua zaidi mmoja wa wananchi hao aliyejitambulisha kwa jina la Mama Silayo amesema  baadhi ya wanawake  wamekuwa wakichapwa kwa fimbo  na askari wa hifadhi ya mlima Kilimanjaro pindi wanapokutwa ndani ya hifadhi wakiokota kuni au kukata majani kwa ajili ya malisho ya mifugo..
 Akijibu tuhuma hizo Kaimu Mkuu wa hifadhi hiyo Bw. Charles Ngendo amewahakikishia wananchi hao kuwa hifadhi hiyo ni salama kwa wale wote walioruhusiwa kuingia  ndani ya msitu wa hifadhi na hawatopata madhara yoyote endapo watatimiza wajibu wao bila kukiuka sheria na taratibu za hifadhi.
Hata hivyo Ngendo amewataka wananchi waliofanyiwa vitendo hivyo wawasilishe malalamiko pamoja  na ushahidi  katika utaratibu rasmi ikiwa ni pamoja na kuonana na uongozi wa hifadhi mapema iwezekanavyo na uongozi hautasita kuwachukulia  hatua watumishi waliotenda vitendo hivyo.
Aidha Ngendo amesisitiza viongozi wa vijiji vinavyozunguka msitu wa hifadhi watumie kamati za mazingira  katika vijiji husika kuratibu namna ya kusimamia wanawake wanaoingia  ndani ya hifadhi  kutafuta mahitaji  waingie kwa usalama bila ya kupata bughudha yoyote kwani maamuzi ya kulinda hifadhi yalipitishwa katika Kikao cha Kamati ya Ushauri ya Maendeleo ya Mkoa (RCC) hivyo utaratibu huo hauwezi kukiukwa.
 Hata hivyo wananchi hao waishio katika wilaya hizo wameishukuru serikali  na hifadhi ya taifa KINAPA kwa kujenga mahusiano mazuri kupitia ujirani mwema ambapo wamekua wakinufaika na mambo mbalimbali yenye tija katika kukuza uchumi na ustawi wa maendeleo ya  huduma za jamii .
  TIZAMA  PICHA ZA MATUKIO MBALIMBALI ZA ZIARA HIYO MUBASHARA.


 Muikolojia wa  Hifadhi ya Taifa ya Kilimanjaro (KINAPA) Imani Kikoti ( wa pili kushoto)
akimuelezea Mkuuu wa Mkoa wa Kilimanjaro Mhe.Anna  Mghwira  mikakati ya hifadhi hiyo katika kuhakikisha uoto wa asili ndani ya hifadhi unalindwa.



Mkuu wa Mkoa wa Kilimanjaro Mhe. Anna Mghwira akiwahimiza  wananchi waishio katika kijiji Ubetu kuendelea kutunza hifadhi ya Taifa ya Mlima Kilimanjaro .
Hawa ni Wananchi wa Kijiji cha  Ubetu ambacho ni moja ya vijiji vinavyopakana na hifadhi ya Taifa ya Mlima Kilimanjaro wilayani Rombo.
TIZAMA PICHA ZA  WANANCHI HAO.
Kushoto ni Mhifadhi ujirani mwema Bi.Hobokela Mwamjengwa akiwa ameongozana na Kaimu mkuu wa Uhifadhi Bw. Charles Ngendo sambamba na Mkuu wa Wilaya ya Moshi Mh.Kippe Warioba.
PICHA ZIFUATAZO ZINAONYESHA WANANCHI WALIOJITOKEZA KUMSIKILIZA MKU WA MKOA NA VIONGOZI WA HIFADHI ILI KUPATA UFUMBUZI WA MAMBO MUHIMU YANAYOHUSIANA NA UHIFADHI.


NA HIZ I NI PICHA ZA MH.MKUU WA MKOA WA KILIMANJARO BI.ANNA MGWHIRA AKIZUNGUMZA NA WANANCHI.




NA ZIFUATAZO NI PICHA ZA WANANCHI WALIOKUA WAKIULIZA MASWALI KWA LENGO LA KUPATA MREJESHO JUU YA UHIFADHI SAMBAMBA NA KUMLAKI MH.MKUU WA MKOA.













































Hakuna maoni:

Chapisha Maoni