Tafuta katika Blogu Hii

Jumatatu, 30 Oktoba 2017

IMANI ZA KISHIRIKINA ZADAIWA KUCHANGIA MATUKIO YA KIKATILI.


Imeelezwa kuwa matukio ya ukatili wa kijinsia unasababishwa na imani potofu za kishirikina zinazochangiwa na matapeli wanaojiita waganga wa jadi na kujihusisha na ramli chonganishi.
Hayo yamebainishwa na wadau wa ulinzi wa watoto kupitia dawati la jinsia na watoto nchini Zanzibar katika ziara ya siku tano mkoani Kilimanjaro katika wilaya ya Hai iliyojumuisha viongozi mbalimbali kutoka nchini humo kwa lengo la kubaini na kujifunza mbinu mbalimbali katika kukabiliana na changamoto za kiukatili dhidi ya watoto.
Ukatili wa kijinsia ni tatizo kubwa ambalo linawanyima uhuru wanaume, wanawake na watoto kufurahia haki zao za msingi ambazo pia ni haki za binadamu.
Wamesema tatizo hili linaonekana zaidi kwa wanawake kutokana na hali duni ya kiuchumi na kutofahamu sheria kuongeza idadi ya wahanga wengi wa ukatili wa kijinsia kimwili, kingono na kisaikolojia.
Kwa upande wake Naibu katibu mkuu wizara ya kazi,uwezeshaji wazee,vijana,wanawake na watoto nchini Zanzibar Hassan Khatibu Hassan amesema  vitendo vya ukatili vinasababisha wanawake kupata maumivu, yanayotokana na vitisho, kunyimwa uhuru mbele ya jumuiya au eneo la faragha.
Akifafanua zaidi amesema ukatili wa kijinsia umegawanyika katika makundi mbalimbali ikiwemo
ukatili wa kimwili “ni matendo anayofanyiwa mwanamke au mwanaume kwa kuumizwa sehemu za mwili wake ikiwemo  shambulio la mwili, kukeketa wanawake, kupiga, kuchoma mwili moto, matumizi ya silaha kwenye mwili, matumizi ya vitu vyenye ncha kali kudhuru mwili, kuvuta nywele, usukuma, kunyonga mkono au mguu, kupiga kichwa au kubamizia ukutani”.
Ukatili wa kisaikolojia” Muathirika wa ukatili wa namna hii hupata maumivu bila watu wengine kutambua kuwa amepata maumivu ambayo humsababishia mtu maumivu ya kihisia na kiakili
mwathirika kuona amedharauliwa na kushushwa adhi yake katika jamii kwa sababu tu ya jinsi yake
mfano matusi kwa njia ya ishara au maneno yenye lengo la kudhalilisha, kutishia kufanya fujo, maneno ya fedheha, dharau au kutishia kutoa siri hadharani, kunyang’anywa watoto kwa makusudi, kuingiliwa faragha, kutishiwa kuuawa, kunyang’anywa watoto kwa makusudi, wivu wa kupindukia.
Ukatili wa kingono” ukatili utokanao na mila na desturi zenye madhara ukatili huu unahusisha masuala ya ngono na mahusiano ya mapenzi iwe katika ndoa au nje ya ndoa Kwa mfano  matumizi ya vitu kama chuma, fimbo, kisu, mti n.k kuingiza kwenye sehemu za siri za mwanamke au mwanamume, kubaka, kujaribu kubaka/jaribio la kubaka, kulawiti (kuingilia kinyume cha maumbile), usafi rishaji/utoroshaji wa binadamu kwa ajili ya ngono, utumwa wa kingono, unyanyasaji wa kingono, bugudha za kingono mfano kutomaswa sehemu za matiti, makalio, kiuno na sehemu nyingine za mwili bila ridhaa, kulazimisha tendo la ndoa hata kama ni wanandoa, ndoa za utotoni, kupima ubikira kwa wasichana, kulazimisha kutoa mimba, kulazimisha kutia mimba, kulazimisha ngono bila kujali maambukizi ya magonjwa kama VVU na UKIMWI na magonjwa mengine ya zinaa na kulazimisha kufanya biashara ya ukahaba.
Aidha Hassan amesema kupitia ukatili wa aina mbalimbali yamekuwa yakisababisha madhara makubwa katika jamii ikiwemo majeraha, ulemavu wa kudumu, vifo, huzuni, msongo wa mawazo, kushindwa kutimiza majukumu ya ulezi, uzazi na uzalishaji, kuharibika kwa mimba, migogoro kwenye familia,kushuka kwa uchumi kutokana na mzigo mkubwa kwenye huduma za afya ya
Umma na kupungua kwa uzalishaji malina hatimaye kulegalega kwa malezi ya watoto. 
                                    TIZAMA PICHA MUHIMU KATIKA TUKIO HILI.