Maadhimisho ya wiki ya nenda kwa usalama yaliyofanyika
kitaifa mjini moshi mkoani Kilimanjaro yamemalizika salama huku wadau mbalimbali
wa vyombo vya moto na watembea kwa miguu wakionyesha kufurahishwa na utendaji
kazi wa jeshi la polisi katika kutoa mchango wao katika kuzuia ajali za
barabarani na kufanikiwa kupunguza idadi kubwa za ajali zinazotokana na uzembe
wa madereva wasiowaaminifu ,ulevi uliokithiri na matumizi mabaya ya alama za
barabarani.
Maadhimisho hayo yamemalizika katika uwanja wa Mashujaa na
kuhusisha wananchi, wadau mbalimbali na viongozi wa umma.
Maadhimisho hayo yamemalizika kwa hari kubwa na uelewa kwa
makundi ya kijamii sambamba na kukabidhiwa vyeti na zawadi mbalimbali kwa
washriki walioshinda michezo mbalimbali ikiwemo mpira wa miguu na matumizi
sahihi ya fasihi andishi kupitia shule za msingi.
Mgeni rasmi katika maadhimisho hayo ni mkuu wa mkoa wa Kilimanjaro Mh.Anna Mghwira ambapo alianza kwa kukagua mabanda ya maonyesho katika sekta mbalimbali na kupata maelekezo juu ya jitihada muhimu wanazozitumia wadau wao katika kuhakikisha wanapunguza ajali za barabarani zinasababishwa na hitilafu mbalimbali na ukiukwaji wa sheria za alama za barabarani.
Mgeni rasmi katika maadhimisho hayo ni mkuu wa mkoa wa Kilimanjaro Mh.Anna Mghwira ambapo alianza kwa kukagua mabanda ya maonyesho katika sekta mbalimbali na kupata maelekezo juu ya jitihada muhimu wanazozitumia wadau wao katika kuhakikisha wanapunguza ajali za barabarani zinasababishwa na hitilafu mbalimbali na ukiukwaji wa sheria za alama za barabarani.
Hakuna maoni:
Chapisha Maoni