“ Maziwa salama chakula na pesa “Kauli hii inachukua nafasi
yake katika kukuza uchumi wa wafugaji na kuboresha afya za watumiaji wa maziwa
salama licha ya waliowengi kulalamikia gharama za kumudu kununua bidhaa hiyo
adimu .
Jambo hilo ni kama anasa kwa
watanzania walio wengi na haoni umuhimu wake kwa upande wa afya mwilini,ukweli
ni kwamba baadhi ya watu wanapuuzia na hawaoni umuhimu wa kunywa maziwa hata
kama yanapatikana kwa urahisi katika maeneo wanayoishi.
Wataalamu wa afya wanasisitiza kuwa
maziwa yana kazi nyingi mwilini ikiwamo kuifanya ngozi kuwa nyororo, kuimarisha
meno na mifupa kutokana na vitamin zilizopo.
Shirika la maendeleo la uholanzi CNV wameamua kuungana na wadau wa maziwa kupitia sekta ya
usindikaji na unywaji wa maziwa salama kwa lengo la kuhamasisha unywaji wa maziwa na kuwakutanisha
wadau mbalimbali kujifunza na kuona
shughuli muhimu zinazofanywa na wengine katika sekta tofauti na kuunda umoja wa
wadau wa maziwa sambamba na kuzindua
jukwaa la unywaji wa maziwa mkoani
kilimanjaro.
Shirika la Afya Duaniani (WHO),
linapendekeza kila mtu anywe angalau lita 200 za maziwa kwa mwaka ingawa
wastani kwa dunia ni lita 108.
Tamasha hilo limeandaliwa na wadau mbalimbali wa
maziwa wakiwemo wafugaji,wasindikaji wa maziwa, vyama vya ushirika na serikali .
Madhumuni ya
tamasha hilo ni kuhamasisha unywaji wa maziwa ,kuwakutanisha wadau mbalimbali
na kuwaleta pamoja kujifunza na kuona shughuli muhimu zinazofanywa na wengine
wa maendeleo katika sekta tofauti na kujua hali halisi ilivyo sasa katika
mazingira tofautitofauti sambamba na kuunda umoja wa wadau wa maziwa na
kuzindua jukwaa la maziwa la mkoa wa kilimanjaro.
Akizungumzia umuhimu wa shirika hilo la CNV meneja mradi Bw.Tom Ole Sikar amesema kazi kubwa ya shirika hilo ni kuwaleta wadau wa maziwa pamoja
,kutatua changamoto zinazowakabili wafugaji hususani katika upande wa masoko kwa wafugaji na kupunguza umasikini
unaosababisha na ufugaji usio na tija kwa kuwajengea uwezo kuwawaezesha kuwapatia elimu juu ya ufugaji
bora kwa kuzingatia lishe bora,maji na
nishati.
Akifafanua zaidi amesema katika tafiti zilizofanyika
katika wilaya ya siha na hai ambapo mradi huo ndipo ulianzia rasmi kuna jumla ya takribani ngombe elfu 53 wa maziwa na
karibu kaya laki140 zinajishughulisha na
uzalishaji wa maziwa ambapo uzalisha takribani lita laki mbili na nusu
kwa siku.
Amesema katika wilaya hizo mbili kuna jumla ya vyama
vya msingi vya maziwa 14 na vikundi 8 vya ushirika vikiwa na jumla ya wanachama 1500 ambapo
kwa umoja wa vyama hivyo kwa siku vinauwezo wa kukusanya lita takribani elfu 24
kwa siku .
Akizungumzia swala la masoko amesema kwa umoja wa
vyama hivyo wamekua na uwezo wa kusindika maziwa salama kwa walaji na
kusababisha swala zima la unywaji wa maziwa kuwa na ongezeko kubwa na kutoa
hamasa kwa walaji.
Hata hivyo akizungumzia changamototo mbalimbali ni
pamoja na mwitikio hafifu kwa wafugaji kutokana na elimu duni juu ya ufugaji
bora ambapo awali wafugaji hao walikua wanazalisha lita 5 -8 kwa siku ambapo kwa
sasa shirika la SNV wameweza kutatua kupitia tafiti za mbegu bora ,ubora wa
malisho,nishati lishe na kuongeza idadi ya uzalishaji wa maziwa kufikia lita
8-12.
Amesema kupitia changamoto hizo shirika hilo
limeweza kuwajengea uwezo wafugaji ,wajasiriamali na wadau wa maendeleo juu ya
ubora wa thamani wa soko la maziwa
ambapo kupitia elimu hiyo wameweza kuyakutanisha
makundi mbalimbali katika jamii na kuwapatia
fursa za ajira kupia sekta ya ufugaji bora,malisho na soko la maziwa.
Hakuna maoni:
Chapisha Maoni