Tafuta katika Blogu Hii

Jumatano, 11 Oktoba 2017

JESHI LA POLISI MKOANI KILIMANJARO LIMEJIDHATITI KUKOMESHA VITENDO VYA KIUHALIFU WA KUTUMIA SILAA.



Imeelezwa kuwa umahiri wa Jeshi la polisi mkoani Kilimanjaro pamoja na uweledi katika kutoa na kupokea taarifa kutoka kwa raia wema umefanikisha kuzuia matukio ya kiuhalifu wa kutumia silaha za moto.
 Akizungumza na waandishi wa habari ofisini kwake kamanda wa polisi mkoani hapa Hamis Issah amesema kupitia askari wa jeshi hilo wamefanikiwa kuzuia tukio la ujambazi kwa kutumia silaa   lililopangwa kufanyika mnamo tarehe 08/10/2017 katika kijiji cha Chilio kilichopo kata ya Holili Tarafa ya Mengwe wilaya ya Rombo katika kiwanda cha Moshi Cement.
Akifafanua zaidi kamanda Issah amesema jeshi hilo lilifanikiwa kumtia mbaroni mmoja kati ya majambazi hao mnamo 05/10/2017 aliyejulikana kwa jina la Robert Paulo Massawe (51)Mchaga mkazi wa Dar es salaam akiwa na silaha aina ya Smg namba 1996AFU 2761 katika maeneo ya kaloleni karibu na kiwanda cha ngozi  na mara baada ya kuhojiwa alikiri kuhusika na matukio mbalimbali ya kiuhalifu na kuliahidi jeshi hilo kulipa ushirikiano kwa kuwapeleka maeneo husika waliopanga kutimiza tukio la kialifu na askari walilazimika kuunda mtego ili kuwadhibiti majambazi hao.
Issah amesema baada ya kufika eneo la tukio  Massawe akiwa amesimama kwa ajili ya kutekeleza uvamizi huo alipowakaribi wenzake aliwataarifu wenzake kwa kupiga kelele  kuwa polisi wapo eneo hilo hali iliyowapelekea majambazi hao kukimbia huku wakiwa wanapiga risasi ovyo kwa lengo la kujihami wasikamatwe na kusabisha kifo chake kutokana na maumivu makali ya risasi zilizompata maeneo mbalimbali ya mwili ikiwemo katika mkono wa kushoto,mgongoni na mguu wa kulia.
Akitaja baadhi ya matukio ambayo alishawai kutekeleza wakati wa uhai wake ni pamoja na 1991-1992 ambapo alikamatwa Tarekea wilayani Rombo kwa kosa la unyang’anyi wa kutumia silaha.
Mnamo 26/06/2012 katika maeneo ya Kyusa jirani na Panone Petrol Station walimvamia mfanyabiashara na kumpora fedha ,29/9/2014 walimvamia mfanyabiashara aitwaye Robart na kumpora fedha pamoja na vocha ,mnamo 26/6/2015 walivamia Holili stand na kumpora fedha mfanyabiashara mmoja na waliuwa watu wawili,3/4/2017walimvamia mfanyabiashara mmoja maeneo ya Himo na kumpiga risasi ya paja kasha kumpora fedha kiasi cha Tsh.million 6,27/4/2017 eneo la Osterbay walimvamia mfanyabiashara akiwa dukani kwake na kumpiga risasi ya kichwa na kumjeruhi mtu mwingine aliyekuwepo pembeni,26/6/2017 maeneo ya woodland walimvamia mfanya biashara na kumpora simu yake pamoja na vocha na mnamo 22/7/2017 maeneo ya mailisita High way Supermarket walimvamia mfanya biashara na kumpiga risasi ya paja kisha kupora simu pamoja na vocha za simu aina mbalimbali.
 TIZAMA PICHA ZA KAMANDA WA POLISI MKOANI KILIMANJARO AKIWAONESHA WAANDISHI WA HABARI BAADHI YA VIELELEZO.
                SIKILIZA SAUTI YA KAMANDA AKIELEZEA VIELELEZO HIVYO.


Hakuna maoni:

Chapisha Maoni