Tafuta katika Blogu Hii

Jumatano, 1 Mei 2019

DKT.MGWHIRA ALIA NA USHIRIKA KILIMANJARO AAGIZA UWAJIBIKAJI KWA WATUMISHI WA UMMA KUPITIA KADA MBALIMBALI.


Pichani aliyeshika kipaza sauti  ni Mkuu wa mkoa wa Kilimanjaro Mhe.Dkt. Anna Mgwhira akisisitiza jambo katika ghafla za sherehe za Mei Mosi mwaka huu(2019).
Mkuu wa mkoa wa Kilimanjaro Dkt.Anna Mgwhira amezitaka Mamlaka ,taasisi na sekta mbalimbali kujitathimini katika kutoa huduma bora kwa walengwa na kuziadhimisha sikukuu ya Wafanyakazi   kama chachu ya kuwatumikia wananchi kwa uadilifu kupitia huduma zilizotukuka .
 Akizungumza katika ghafla za sherehe ya Mei  Mosi ziliyofanyika kimkoa katika viwanja vya Chuo kikuu  cha Ushika mjini Moshi  (MOCU)ameeleza kufurahishwa na sherehe hiyo iliyovikutanisha vyama mbalimbali vya Wafanyakazi,Taasisi za Umma ,Mashirika Umma  na Wajasiriamali .
Mghwira  amesema mbali na kuwepo kwa  fursa za ajira mkoani Kilimanjaro  Vyama vya ushirika vimekua ndio chanzo cha kudhorota kwa sekta  mbalimbali za kiuchumi ikiwemo kilimo na biashara licha ya kuwepo kwa changamoto kubwa iliyosababishwa na kufa kwa viwanda vilivyokua vikitoa ajira kwa wananchi wengi .
“ushirika ndio umeua viwanda Kilimanjaro,Ushirika ndio umeua Mashamba ya Umma Kilimanjaro,Ushirika ndio umesababisha kuyumba kiuchumi kwa benki ya Ushirika na kupelekea kutofanya kazi kwa faida takribani miaka miwili sasa  licha ya kuwepo kwa wasomi Maprofesa katika Ushirika  , kazi ni ushuhuda ndugu zangu”amesema mkuu huyo.
Akifafanua zaidi amesema kupitia hilo serikali imekua na mikakati thabiti ya kuboresha miundombinu rafiki ya uwekezaji katika mkoa huo kupitia sekta jumuishi na kupanua wigo wa ajira kwa wazawa sambamba na kukabiliana na uharibifu wa mazingira unaosababishwa na shughuli za kibinaadamu ili kulinda rasilimali za taifa zinazopatikana ndani ya mkoa ikiwemo uwepo wa uoto wa asili unaoitangaza  nchi yetu katika soko la utalii.
Katika hatua hiyo Dkt. Mgwhira  amewatunuku vyeti na zawadi mbalimbali baadhi ya wafanyakazi kupitia kada mbalimbali kama moja ya alama ya uwajibikaji na utekelezaji wa majukumu yao wanapokua kazini.
Sherehe hizi za Mei mosi  zinalenga kuwakumbuka baadhi ya wafanyakazi duniani waliopata kadhia mbalimbali wakiwa katika majukumu ya kutekeleza  wajibu wao  ambapo kauli mbiu kitaifa mwaka huu ni “TANZANIA YA UCHUMI WA KATI INAWEZEKANA ,WAKATI WA MASLAHI BORA KWA WAFANYAKAZI NI SASA “
FUATILIA KWA UMAKINI MTIRIRIKO WA TUKIO ZIMA; HAYA NI MAANDAMANO YA      WADAU.
Mhe.Mkuu wa mkoa akizungumza jambo na Mratibu wa TUCTA mkoa Bi.Digna Nyaki katikati ni Kaimu Mwenyekiti wa TUCTA Bi.Winnie Swai.

Dkt.Anna Mgwhira akisisitiza  umuhimu wa wafanyazi kujitathimini katika kuyfikia malengo"Umahiri wa utendaji kazi ni ni matokeo yanayopelekea ushuhuda wa kazi yako.
Pichani aliyevaa T.sheti nyekundu ni Mkuu wa Wilaya ya Rombo Mhe.Agness Okororo na anayefuatia ni Mhe.Rosemary Senyamule mkuu wa Wilaya ya Same.
 
 


Wadau mbalimbali wakifuatilia kwa umakini maandamano hayo.


 

 

 
 

 
PICHA ZIFUATAZO NI ZA WADAU KUTOKA HOSPITALI YA RUFAA MAWENZI WAKICHANGIA HUDUMA YA DAMU SALAMA.