HABARI SPECIAL

Tafuta katika Blogu Hii

Jumatatu, 29 Aprili 2019

HALIMASHAURI YA MOSHI IMEANZISHA KAMPENI NYAKUANYAKUA YA KUKAMATA MIFUGO INAYOACHIWA OVYO KWA LENGO LA KUTUNZA MAZINGIRA KWA TIJA.

Conversation opened. 1 unread message.
Halimashauri ya Wilaya ya moshi mkoani Kilimanjaro imeanzisha kampeni mpya ambayo itasaidia kudhibiti uhifadhi wa mazingira kupitia shughuli zinazofanywa na binadamu na kuchangia uharibifu wa  mazingira hususani kwa wafugaji wanaoachia mifugo yao ovyo  inayoharibu miche ya miti inayoendelea kupandwa na serikali na wadau wa mazingira wilayani humo.
Akizungumza  kwa niaba ya Mkuu wa Wilaya ya Moshi ,Angelina Marko ambaye ni katibu tawala wa wilaya hiyo wakati wa ghafla ya  uzinduzi wa zoezi la upandaji miti wilaya humo katika  shule ya msingi Mabungo kata ya kirua kusini moshi vijijini amesema utunzaji wa miti ni zoezi endelevu ambalo kila mwananchi anapaswa kuhakikisha anaunga mkono jitihada muhimu zinazofanywa na Serikali na wadau wa mazingira katika kulinda uoto wa asili.
 “Haiwezekani serikali na wadau wa mazingira waweke jitihada za kupanda miti hatimaye mifugo ije nakuharibu ,watachukuliwa hatua watakao achia mifugo yao itakayosababisha uharibifu wa miti inayopandwa, zipo sheria zilizowekwa za vijiji na wilaya katika kudhibiti mifugo itakayosababisha uhariifu wa mazingira.”alisema
Akifafanua zaidi  amesema kampeni hiyo imeanzishwa kwa tija ili kukamata mifugo ambayo itakua inazurura ovyo na kusababisha uharibifu wa miche ya miti inayoendelea kupandwa wilayani katika maeneo mbalimbali Wilayani humo,ambapo mnyama yeyote atakayekamatwa atatozwa fine ama kupelekwa mnadani ili kukomesha uharibifu huo.
Akizungumzia kuhusu hali  halisi ya mazingira kwa sasa amesema  imebadilika kutokana na kuwepo kwa uharibifu wa mazingira na imepelekea kupungua kwa theluji ya Mlima Kilimanjaro ambapo wataalamu wanasema imebakia 18.2% jambo ambalo linaweza kusababisha kupungua kwa soko la utalii wa watalii watakaotembelea mlima huo.
“Tumekua tukifanya jitihada hizi za kupanda miti maeneo mbalimbali ya wilaya yetu tangu mwaka( 2014) hadi sasa (2019) lakini je ufuatiliaji unakuaje baada ya kupanda miti hii ,ningetoa hamasa kwa viongozi wenzangu na wadau wa mazingira tuwe tunahakiki miti tunayoipanda na kutembelea kila baada ya muda  ili kujua maendeleo.”alisema Angelina ambaye pia amechangia miche ya miti 500.
Wakizungumza kwa nyakati tofauti wananchi walishiriki zoezi hilo la upandaji miti katika  eneo la shule ya Mabungo,wamesema wanaunga mkono jitihada za Serikali katika kupanda na ,kulinda  mazingira kwani miti hiyo inafaida mbalimbali kama kuwaletea mvua  pamoja na hewa nzuri .
Kwa upande wake  Mwenyekiti wa halimashauri hiyo Bw. Michael Kilawila  amesema upandaji wa miti ni njia mojawapo ya utunzaji mazingira kwa lengo la kulinda uoto wa asili pamoja na kukabiliana na mabadiliko ya tabia nchi yanayoweza kujitokeza endapo uharibifu wa mazingira utatokea na kujinasibu na baa la njaa .
“Baadhi ya wananchi hawafahamu umuhimu wa miti, lakini ukweli ni kwamba miti hii ni lulu ambayo tunapaswa kuilinda kwani sisi tunaitegemea hewa tunayoivuta inatokana na miti hii sambamba na kuleta unyevu katika mimea tunayoiotesha.”alisema Kilawila
Akisoma taarifa ya upandaji miti wilaya ,Afisa misitu wa wilaya hiyo ya Moshi,Joshua Mungure amesema halimashauri hiyo imekua ikipanda miti kila mwaka hususani kipindi vya mvua za masika na vuli kwa lengo la kuhamasisha wananchi na wadau kutumia mvua zinazazoendelea kunyesha kupanda miti.
Amesema licha ya kuwepo kwa mafanikio katika upandaji miti bado kuna changamoto kwa  baadhi ya wananchi wasio na uelewa juu ya utunzaji wa mazingira,ambao hukata miti ovyo maeneo ya misitu ,ulishaji na uchungaji wa mifugo maeneo ya hifadhi na tambarare na kwamba utatuzi wa changamoto hizo elimu imeendelea kutolewa kwa wananchi juu ya utunzaji wa mazingira ili kuepusha uharibifu huo. 
Hata hivyo kwa upande wake mwalimu Mkuu wa shule hiyo ya msingi Mabungo iliyofanyika uzinduzi huo wa kupanda miche hiyo Bw. Robert Materu amesema imepandwa miti 320 katika eneo la wazi la shule hiyo huku akishukuru  uongozi wa wilaya kwa kufanya uzinduzi huo shuleni hapo na kwamba watailinda miti hiyo ili iweze kukua na kustawi.
Halimashauri hiyo ya Moshi imeanza zoezi hilo kwa kuanza kupanda miti 320 katika shule hiyo kati ya miti 1000 iliyokua inatakiwa kupandwa ambapo wilaya hiyo kwa mwaka huu inatarajia kupanda 9000 maeneo mbalimbali yanayozunguka mlima Kilimanjaro.





Posted by @habarispecial.blogspot.com at 4/29/2019 09:49:00 PM
Tuma Hii kwa Barua pepeBlogu Hii!Chapisha kwenye XShiriki kwenye FacebookShiriki kwenye Pinterest
Chapisho Jipya Taarifa za zamani Nyumbani
  • HABARI SPECIAL

Tafuta katika Blogu Hii

HABARI ZILIZOGONGA VICHWA WIKI HII

  • RC KAGAIGAI AWAFUNDA WAKUU WA WILAYA WATEULE KILIMANJARO#KASIMAMIENI UTA...
  • DKT MGWHIRA ALIVYOTINGA MAKANISANI#KILIMANJARO TUPO SALAMA TUJIDHATITI N...
  • RAIS MAGUFULI LIVE AKIFUNGUA MKUTANO MKUU WA CCM 2020
  • WAZIRI MBARAWA AFUNGUKA MENGI SEKTA YA MAJI KILIMANJARO
  • LIVE: RAIS DK. JOHN P. MAGUFULI AWAAPISHA VIONGOZI WATEULE, IKULU CHAMWI...
  • SERIKALI YAAHIDI KUTUMIA BUSARA KUUMALIZA MGOGORO BAINA YA SBL NA RAHCO.
  • RC KILI ACHARUKA KAMA UNAUPENDA MCHEPUKO UKATIE BIMA YA AFYA
  • Harmonize - Magufuli (Official Video) Sms SKIZA 8547071 to 811

MITANDAO MINGINE

  • Father Kidevu
    MTUHUMIWA MAKOSA NANE YA KIKODI AFIKISHWA MAHAKAMANI
    Saa 2 zilizopita
  • TAIFA LETU.com
    CHUKUA HII: WANASAYANSI, WASOMI NA WAVUMBUZI WENGI WALIKUWA NI 'VICHAA'
    Miaka 9 iliyopita
  • JAIZMELALEO
    SPORTS UPDATE: Emile Heskey atupia dhidi ya Blackburn
    Miaka 11 iliyopita

BOFYA HAPA KWA HABARI NYINGINEZO

THE HOUSE OF INFORMATION 0782917091

@habarispecial.blogspot.com
Tazama wasifu wangu kamili
Powered By Blogger

READERS ON LINE NOW

Translate

Mandhari ya Alama maalum. Inaendeshwa na Blogger.