Tafuta katika Blogu Hii

Jumapili, 27 Julai 2014

MAPIGANO YALIPUKA BENGHAZI



Watu wasiopungua 38,wengi wao wakiwa wanajeshi wameuwawa katika kipindi cha masaa 24 yaliyopita kufuatia mapigano makali kati ya jeshi la Libya na wanamgambo wa Kiislam katika mji wa mashariki wa Benghazi-maafisa wa serikali wamesema. 

Familia kadhaa zinayapa kisogo maskani yao. Duru za kijeshi zimesema mapigano yameripuka jana pale makundi ya itikadi kali yalipoyashambulia makao makuu ya kikosi maalum cha jeshi karibu na eneo la kati la Benghazi na kusababisha hasara miongoni mwa wanajeshi waliokuwa wakizihami kambi zao.

Hospitali kuu ya Benghazi imesema miili 28 ya wanajeshi imepelekwa katika hospitali hiyo katika kipindi cha masaa 24 yaliyopita,pamoja pia na majeruhi 50 huku miili ya wanajeshi wengine 2 na majeruhi 10 wakipelekwa katika hospitali ya Al-Marj iliyoko kilomita 100 mashariki ya Benghazi. Msemaji wa baraza la mapinduzi-linaloyaleta pamoja makundi tofauti  ya itikadi kali amesema wamewapoteza wapiganaji wao wanane. 

Baraza la mapinduzi linadai kuhusika na mashambulio kadhaa katika eneo hilo la mashariki ya Libya.

Hakuna maoni:

Chapisha Maoni